POLISI NCHINI KUCHUNGUZA TUKIO LA KUTEKWA KWA MCHUNGAJI

 

Jeshi la Polisi limeeleza kushangazwa na taarifa za kutekwa kwa Mchungaji Yanick Mbombo Cele raia wa Kongo jijini Dar es Salaam.

‎Mchungaji Yanick Mbombo alikamatwa Mei 15, 2025 mkoani Iringa kwa tuhuma za ubakaji na mauaji ya watoto wadogo, lakini ushahidi haukujitosheleza hivyo hakuandaliwa mashtaka.


‎Juni 17, 2025, Mchungaji na wenzake walifikishwa mahakamani kwa mashtaka ya kuendesha genge la uhalifu na kujipatia kesi kwa njia za udanganyifu, na walikiri kosa kwa njia ya Plea bargain.
‎ Watuhumiwa walilipa faini ya shilingi milioni 20 na magari yao yakataifishwa, huku Mchungaji Yanick akiondolewa nchini na hakutakiwa kurudi tena.



‎ Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kuhusu taarifa za uwepo wa Mchungaji nchini na kutekwa kwake, na linaomba yeyote mwenye ushuhuda awasilishe kwenye kituo cha Polisi.

Chapisha Maoni

0 Maoni