POLISI LIMEANZA UCHUNGUZI KUWATAFUTA WATU WALIOMUHAMASISHA MTOTO KUVUTA SIGARA

 


Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi na kuwafuatilia watu wanaohusika na vitendo vya kikatili dhidi ya mtoto.

‎Polisi wanatoa wito kwa yeyote anayewafahamu watu hao au mtoto huyo kusaidia katika kumfikia na kuokoa afya ya mtoto.

‎Polisi wanatoa onyo kwa watu wenye tabia za unyanyasaji kwa watoto kwa lengo la kutafuta wafuasi kwenye mitandao ya kijamii, wakisema hawatasita kuwakamata.

‎ Picha za mtoto akihamasishwa kuvuta sigara zinasambazwa mitandaoni, kitendo ambacho ni kinyume cha sheria na kanuni za kijamii na nchi.

Chapisha Maoni

0 Maoni