Na Mwandishi wetu-Dodoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Mhe. William Lukuvi, ameongoza kikao maalum cha maandalizi kuelekea maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani yanayotarajiwa kufanyika tarehe 1 Desemba 2025.
Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dodoma na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Dkt. James Kilabuko, na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) Dkt. Samwel Sumba.Katika kikao hicho, viongozi hao walijadili hatua za mwisho za uratibu, mbinu za kuongeza uhamasishaji kwa jamii, na kuhakikisha kuwa ujumbe wa maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani unawafikia wananchi kwa ufasaha na kwa wakati.
Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani hufanyika kila mwaka ili kuongeza mwitikio katika mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya VVU, kupunguza unyanyapaa, na kuimarisha upatikanaji wa huduma kwa watu wanaoishi na VVU.


0 Maoni