AHUKUMIWA MIAKA 20 JELA KWA SHAMBULIO LA AIBU

Mahakama ya Wilaya Temeke Jijini Dar es Salaam  imemukumu kutumikia kifungo cha miaka 20 jela Rashidi  Ruambo mwenye umri wa miaka 56  fundi ushonaji mkazi wa Yombo Makangarawe kwa kupatikana na hatia ya kosa la Shambulio la aibu

 Hukumu hiyo imeitolewa Novemba 25,2025 na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Temeke Mh. Janeth Kaluyenda akisoma hukumu hiyo amesema kuwa  Mahakama imeridhika na ushahidi  uliowasilishwa Mahakamani hapo ambao pasi na chembe ya shaka umemtia hatiani mtuhumiwa huyo.


Imeelezwa kuwa mnamo mwezi  Novemba 24,2024 majira ya saa 06:00 mchana huko maeneo ya Yombo Makangarawe mtuhumiwa akiwa katika duka lake la ushonaji  alimuita mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 6 mwanafunzi wa chekechea na kuanza kumchezea  kwa kumuingizia vidole sehemu zake za uke na kisha mtoto huyo akaenda kumueleza mama yake juu ya kitendo hicho alichofanyiwa.

Chapisha Maoni

0 Maoni