Maxence Melo Mubyazi ni Mkurugenzi wa Jamii Forums na Jamii Africa amechapisha ujumbe kupitia ukurasa wake wa Instagram kuwa ofisi za Jamii Forum zilizopo Mikocheni Jijini Dar Es Salaam zimefanyiwa uvamizi muda mchache uliopita Leo hii Septemba 5.
Max amesema uvamizi huo umefanyika huku lengo ikiwa ni kumtafuta yeye. Huku akienda mbali zaidi na kusema kuwa ataweka ukweli hadharani hivi karibuni.
Max hajaeleza wazi kuwa ni kina nani hasa wamehusika na uvamizi huo.

0 Maoni