KIVULI NDANI YA MWILI { SEHEMU YA KWANZA }

Ingawa mvua kubwa sana ilinyesha mchana wa siku hiyo, bado haikutosha kubadili hali ya jiji la Dar es salaam. Joto lilikuwa kali kupita kiasi usiku wa siku hiyo, wakazi wa maeneo ya Tabata Kimanga walilazimika kulala nje ya nyumba zao! Yote hii ikiwa ni kulikimbia joto lililokuwemo ndani ya nyumba zao.

         Hiyo ndiyo ilikuwa hali ya Dar es salaam kwa usiku huo.Tayari ilishagonga saa kumi na moja alfajiri, adhana za misikiti mbali mbali zilisikika kuwaamsha na kuwaimiza waumini wa kiislamu kuwai katika nyumba za ibada kwa ajiri ya kufanya ibada.

          Miongoni mwa msikiti uliokuwa unapiga adhana ni msikiti wa Almasjid Tidc wa Tabata Mawenzi eneo la kituo cha chama, baada ya kupigwa adhana hiyo waumini walifika na kuongezeka kadri muda ulivyozidi kusogea.

          Lakini chakushangaza Imamu Shafii wa kuongoza ibada  alikuwa aonekani hapo Msikitini. Waumini wa kiislamu walijipa Moyo yupo eneo hilo hilo la msikiti, lakini hadi muda wa ibada unatimia Imamu Shafii alikuwa aonekani.

"Ni nani aliepiga adhana?"

          Ni swali lililoulizwa na mmoja wa waumini wa kiislamu waliopo hapo msikitini, lakini hakuna aliejitokeza katika kundi lao kuthibitisha yeye ndie alipiga adhana. 

Wakiwa wanashauriana nani aongoze ibada kwakua muda wa ibada umeshatimia, mmoja wa waumini anaona damu kibla anawaonesha wenzake, wanasogea na kuanza kuangalia hizo damu.

“Damu hii ya nini?”

          Muumini mmoja anauliza huku anawaonesha waumini wenzake hiyo damu, walipepesa macho huku na huko labda wataona kiumbe chochote kilichokufa lakini wapi mara inasikika sauti kutoka mlangoni.

“Mashekhee njooni nje”

Walitoka hadi nje, kama hatua kumi na tano kutoka mlango wa kuingia ndani ya msikitini.

“Ebu angalieni”

Huyo muumini aliwaonesha waumini waliotoka ndani ya msikiti, damu iliojaa sehemu moja.

“Ndani ya msikiti kibla kuna damu kama hii, dhaili kabisa inaonesha damu hii ya binadamu lakini ni ya nani?”

"Swali ilo! kila mtu anataka kujua” 

“Aliepiga adhana ni nani?”

“Tangu tumefika atujamuona aliepiga adhana?”

“Wote atujui?”

“Nani wa kwanza alianza kufika msikitini?”

“Mimi nimefika baada ya dakika kumi adhana ya kwanza kuisha kuadhiniwa ila aliepiga adhana sijamuona”

“Nani sasa kapiga adhana”

          Kwa hakika hakuna aliejua aliepiga adhana wala kufahamu damu hiyo imetokana na nini. Lilikuwa fumbo lililotanda mawazoni mwao bila kulipatia ufumbuzi.

“Cha umuhimu tufanye uchunguzi eneo lote la msikiti”

“Sijui kama tutafahulu kwa hilo kwa sababu damu ipo sehemu mbili kibla na hapa nje”

          Mmoja wa waumini aliwaambia wenzake na kupinga wazo alilotoa muumini mwenzake la kufanya uchunguzi ili kujua chanzo cha damu hiyo ni nini na ya nani.

“Sawa damu ipo sehemu mbili, lakini itakua vizuri tukifanya uchunguzi tunaweza kugundua chanzo cha damu na ya nani”

“Kweli! kabisa!”

          Baadhi ya waumini walimuunga mkono muumini mwenzao anaetoa wazo la kufanya uchunguzi eneo lote la msikiti. Hata muumini aliekuwa anapinga na kwenda kinyume na waumini wenzake alikubaliana nao maana wengi wape. Walianza kufanya uchunguzi eneo la msikiti, baadhi waliingia ndani ya vyoo na wengine walizunguruka nyuma ya msikiti ambako kuna eneo kubwa la kupaki magari.

**********

“INAL LILLAH  WAINA ILAIY RAJUUN”

         Sauti hiyo ilisikika kutoka umbali mrefu na kupenya masikioni mwa waumini wanaofanya uchunguzi eneo la  msikitini ili kujua chanzo cha damu na ya nani. Wote waliacha kazi wanayofanya ya uchunguzi wanasikiliza kwa umakini sauti hiyo inaposikika. Sauti ilizidi kusogea hapo msikitini kutokea kituo cha chama, waumini wanaulizana.

"Sauti ya nini?"

“Ebu tusikilize kwa umakini”

          Walitegesha masikio kama sungura aliehisi hatari, walisikiliza lakini ilikuwa ngumu kujua kwa sababu sauti ilikuwa inasikika kutoka umbali mrefu. Walitoka sehemu walipo walisogea eneo la mlangoni ili kujua sauti ya nini na nani.


“INAL LILLAH  WAINA ILAIY RAJUUN”

          Sauti ya Muumini mmoja ilisikika ikitamka kwa sauti baada ya kusikia sauti hiyo ikitamkwa kutoka kwa mtu huyo anaekuja eneo ilo la Msikiti, anasababisha wenzake kuwa katika mshangao baada ya kutamka.

“Inal lillah  waina ilaiy rajuun, ndio sauti ninayoisikia,”

Wote walishangaa, muumini mmoja alirudia kutamka.

“INAL LILLAH  WAINA ILAIY RAJUUN!!"

"Ndio"

          Muumini huyo aliwaambia waumini wenzake watoke nje, walitoka hadi nje uso kwa uso na muumini mwenzao akitamka kwa sauti ya juu.

“ INAL LILLAH  WAINA ILAIY RAJUUN”

Alifika hadi kwa waumini wenzake akiwa anahema, jasho linamtiririka. 

“ASALAM ALEYKHUM”

"Waleykhum mssalaam"

          Nafsi ya kila muumini ilikiri wazi kuwa na shahuku yakutaka kujua sababu ya kutamka neno  ilo zito la inal lillah  waina ilaiy rajuun.

“Shekhee kulikoni utokapo?”

Muumini mmoja alimuuliza huyo muumini lakini bila kutoa jibu aliingia ndani ya msikiti.

“Nini kimetokea juu yake?”

“Kimemkuta nini muumini mwenzetu?”

“Itakuwa umemfika msiba nyumbani kwake ndio maana yupo katika hali hiyo"

“Kwa uhakika twende tukapate wasaha wake lakini hapa tutabuni kila jambo na kusahau  tatizo tulilokuwa nalo”

          Walikubaliana kwa pamoja walienda hadi ndani ya msikiti walimkuta muumini mwenzao akiwa anasujudu huku akitamka maneno yale yale.

“INAL LILLAH  WAINA ILAIY RAJUUN”

          Wanashangaa kitendo anachokifanya muumini mwenzao, ndipo mmoja wa waumini anamsogerea hadi sehemu alipo.

“Shekhee unachokifanya unakufuru"

Huku anamzuia, huyo muumini anaacha kusujudu, muumini mwenzake anamkarisha kitako. 

"Ebu tuambie kimekukuta nini huko utokapo?”

          Huyo muumini huyo aliedelea kutamka kauli ile ile inallilah waina rajuun mara alianza kuweweseka kama mtu alieingiwa na pepo mbaya. Waumini wenzake wanamkamata wanammbeba juu juu hadi nje sehemu ya kutia hudhu wanamkarisha kitako, muumini mmoja anachota maji anayasomea, alipomaliza kuyasomea anammwagia kichwani huyo muumini. 

          Huyo muumini alipiga kelele moja ya juu huku sura anaangalia mbingu, mara taratibu anainamisha sura chini anaangalia ardhi anakuwa kimya kama dakika tatu, inasikika sauti ya kihemo akipumua kama mtu aliekimbia umbari mrefu, mara anaanza kulia kwa sauti ya chini.

“Shekhee nini tatizo?”

Waumini wenzake walimuuliza, huyo muumini anainuka akiwa na simanzi tele usoni kwake, anamsogerea kila muumini anamshika mabega.

“Imamu Shafii atunae duniani”

           Kila muumini anapopata taarifa hiyo akuweza kuamini anachoambiwa kwa wakati huo, alikuwa anauliza ili kupata uhakika.

“Nini?”

“Imamu Shafii?”

“Amekufa?”

“Ndio amekufa kwa ajari ya Pikipiki na Maiti yake ipo darajani”

“Inal lillah waina ilaiy rajuun"

          Ndio kauli iliosikika katika kila kinywa cha muumini aliopata taarifa ya kifo cha Imamu Shafii. Taarifa hiyo ya kifo Imamu Shafii ghafla unabadili msimamo wa kujua damu walizoziona hapo msikitini kama barafu juani.

          Uzuni inatawara miongoni kwa kila waumini wa msikiti wa Almasjid Tidc kutokana na kifo cha Imamu Shafii. 

          Dakika ishirini na tano, waumini waliungana kwa pamoja walielekea moja kwa moja hadi darajani katikati ya kituo cha Chama na Dukani ndipo ilipo maiti ya Imamu Shafii.

          Ulikuwa mwendo wa dakika tatu, kutoka msikitini hadi hapo darajani ilipo maiti ya Imamu Shafii, kama unavyojua mwendo wa waislamu wakiwa katika msafara wao. Walifika ilipo maiti ya Imamu Shafii wanathibitisha kweli amekufa kwa ajari ya pikipiki. 

          Kila muumini roho ilimuuma sana, wengine walishindwa kuvumilia machozi yaliwatiririrka na wengine walijitenga pembeni huku wakitafakari ajari hiyo Imamu Shafii alikuwa anatoka wapi hadi akapata ajari hiyo kwa sababu nyumbani kwake ni kituo cha Shiba ukiwa unatoka mjini mkono wa kulia, ukiwa unatoka Tabata Kimanga mkono wa kushoto katika mtaa unaelekea nyumba ya wageni J.M,  nyumba ya tatu baada ya kuivuka nyumba ya Mzee Mashindano na mtaa unaotokea katika Pub ya Hassani Mbiligenda almaharufu MPOGORO PUB, nyumba hiyo anayokaa Imamu Shafii almaharufu kwa Mzee Shobo.

          Walitafakari juu ya ajari hiyo Imamu Shafii alikuwa anatoka wapi, anaenda wapi na kwa muda gani lakini bila majibu na wakikukmbuka damu walizoziona msikitini ndio kabisa, lilikuwa fumbo waliloshindwa kulipatia ufumbuzi.

**********

          Taarifa za kifo cha Imamu Shafii zilienea kila kona ya Tabata Kimanga. Mke wa Imamu Shafii nae alipata taarifa za kifo cha mume wake kutoka kwa waumini wa kiislamu. Kutokana na umaarufu wa Imamu Shafii kila aliepata taarifa za kifo chake alifika katika tukio ili kujishuhudia mwenyewe. Watu walitoka sehemu mbali mbali za Tabata Kimanga na kuja katika tukio hilo la ajari. Kila muda ulivyozidi kwenda watu walizidi kuongezeka katika tukio hilo la ajali maeneo ya Darajani.

          Karibu kila aliefika katika tukio hilo la ajali alisikitika baada ya kuona ajali hiyo, lakini kama unavyojua kwenye wengi kuna mengi, wengine wakiwa wanasikitika kutokana na ajali hiyo dereva pikipiki kuungua yeye na pikipiki yake huku Imamu Shafii kichwani akiwa ametapakaa damu ikiashiria amepasuka kichwani lakini wengine walikuwa na kazi ya kupiga picha na kurekodi video na kusambaza katika mitandao ya kijamii.

Waumini wa kislamu awakupendezewa na  kitendo hicho, wanawazuia watu kupiga picha na kurekodi video lakini inakuwa ngumu kwa sababu watu wengi wanazuia huku kule wanapiga picha na kurekodi video. Kama unavyojua tabia za wabongo kila tukio kwao dili ilimradi kujipatia pesa katika mtandao wa youtube na kuchangamsha katika magroup yao ya whatsApp.

**********

                 Askari wa kibongo kama unavyowajua wao siku zote katika matukio wanakuwa wa mwisho kufika na wa kwanza kutaka kujua chanzo cha tukio. Walifika katika tukio walipima ajali na kupiga picha tukio zima la ajali na kuanza kuhoji watu wawili watatu ili kujua chanzo cha ajali lakini kila waliemuhoji aelewi chochote juu ya ajali ilivyotokea na chanzo chake, kila mmoja ameikuta kama ilivyo.

          Unakuwa wakati mgumu kwa askari kujua ilivyotokea ajali hiyo wala chanzo cha ajali hiyo kwa sababu hakuna alieshuhudia wala kuona ajali hiyo ilivyotokea.

"Bebeni maiti zote tuzipeleke hospitali"

           Ni kauli ya mkuu wa kituo akiwaambia askari waliochini yake. Askari walitii amri ya kiongozi wao walisogea zilipo maiti ili wazibebe lakini wakiwa wanaibeba maiti ya  Imamu Shafii ghafla waliibwaga chini.

“Mbona mnaibwaga maiti?”

          Mkuu wa kituo anawauliza askari wake,askari wakiwa kimya wanaiyangalia maiti ya Imamu Shafii huku wakiwa wametawariwa na hofu.

“Tatizo nini?”

          Mkuu wa kituo aliuliza kwa mara ya pili ndipo askari bila kuongea chochote alionesha kwa ishara katika mkono wa Imamu Shafii. Mkuu wa kituo alisogea hadi katika maiti ya Imamu Shafii ili kuangalia anachooneshwa ndipo aliona katika mkono wa Imamu Shafii katika mkono wa kulia, kidole cha shahada kinatoa shahada huku mbele kikiwa na maneno yalioandikwa kiarabu yakisomeka.

"Ash haduanlaa ilaha inlaalha waashhadu anaamuhammada rasuululhaa"

          Kidole cha shahada kikigusa neno moja na lingine. Mkuu wa kituo alishtuka baada ya kuona tukio hilo, alibaki amekodoa macho kama panya kabanwa na mlango. Ilikuwa mara yake ya kwanza katika maisha kuona tukio kama hilo.  

   Hofu ilimtawala, taratibu anarudi nyuma hatua tatu na kusimama bila kujua nini afanye. Askari na wao wanarudi nyuma hadi sehemu aliposimama mkuu wao.

          Raia waliopo hapo waliona tukio hilo mwanzo hadi mwisho. Walisogea ili kuangalia vizuri. Mtu mmoja alitoka nyuma ya kundi la watu huku alitoa simu mfukoni alisogea hadi mbele karibu na maiti ya Imamu Shafii aliwasha kamera anapiga picha lakini kabla frash ya simu aijatoa mwanga wa kamera inazibwa na mkono.

          Huyo mtu aliokuwa anapiga picha alishangaa anageuka kumuangalia alieziba kamera yake ya simu uso kwa uso na mtu akiwa amevaa kanzu nyeupe kama mtu bara la Asia, sura ya huyo mtu ilifanana na sura ya maiti ya Imamu Shafii alishtuka.

          Huyo mtu aliofanana na maiti ya Imamu Shafii ilimpa ishara huyo mtu aliekuwa anataka kupiga picha ishara ya kumkataza kupiga picha. Huyo mtu aliokuwa anataka kupiga picha alishindwa kujua  ni pacha wa maiti ya Imamu Shafii au ni nani maana wamefanana kila kitu. Huyo mtu alietaka kupiga picha alitaka kuongea.

“Shiiiiiiiiiiip”

          Kwa sauti ya chini mtu huyo aliefanana na maiti ya Imamu Shafii alimzuia kuongea chochote. Huyo mtu alietaka kupiga picha alibaki kimya huku anatetemeka mwili kwa uoga. Mtu huyo aliefanana na maiti ya Imamu Shafii alitoa mkono katika kamera ya huyo mtu alietaka kupiga picha na alimwangalia kwa muda kama alitaka kumwambia kitu, mara aligeuka alipiga hatua kutoka katika kundi la watu lakini mbele alisimama anageuka anamnyooshea kidole cha shahada huku akiwa anakichezesha kwa kukikunja na kukinyoosha na aliongea sauti ya chini iliyopenya masikioni mwa huyo mtu alietaka kupiga picha maiti ya Imamu Shafii.

“Ondoka haraka”

          Huyo mtu alietaka kupiga picha maiti ya Imamu Shafii anapita katikati ya kundi la watu anaondoka eneo ilo la ajali. Huyo mtu aliefanana na maiti ya Imamu Shafii, baada ya kuhakikisha huyo mtu alietaka kupiga picha katika maiti ya Imamu Shafii kuondoka na yeye taratibu anapiga hatua anaondoka.

**********

          Muumini mmoja katika ilo kundi la waumini waliokuwepo hapo katika hiyo ajali alienda hadi katika maiti ya Imamu Shafii anaushika mkono wa Imamu Shafii na kuanza kuusomea hadi hicho kidole cha shahada kinatulia kinaacha kutoa shahada. Muumini huyo baada ya kufanikisha hilo anaangalia juu.

“Inshallah”

          Baada ya kutoa kutoa shukrani kwa mwenyezi mungu muumba mbingu na ardhi na mtawala wa mbingu na ardhi na vyote vilivyopo ndani yake.

"Mnaweza mkaubeba kwa sasa"

Mkuu wa kituo aliwaamrisha askari wake wabebe maiti, askari walisogea ilipo maiti ya Imamu Shafii wakiwa wametawariwa na hofu wanaubeba mwili wa Imamu Shafii wanauingiza ndani ya gari walilokuja nalo na wanamalizia kubeba mwili wa dereva bodaboda wanaondoka. 

          Zilibaki stori midomoni ilikuwaje na chanzo chake lakini kila mmoja akuweza kufumbua fumbo la ajali hiyo na dereva wa bodaboda akuweza kujulikana kutokana na kuungua moto mwili wote ila Imamu Shafii alijulikana kwa haraka, zilibaki simanzi na majonzi kwa waumini wa kiislamu Almasjid Tidc  na watu wanaomfahamu.


**********

          Saa tatu juu ya alama, daktari Mbaga, daktari bingwa wa uchunguzi wa maiti katika hospitali ya Amana alishuka katika bajaji anaingia ndani ya hospitali. Alitembea mwendo wa haraka kuashiria kuna kitu anawahi, mkononi akiwa ameshika begi jeusi. 

          Alipofika geti kubwa la kuingia ndani ya hospitali ya Amana alisikia anaitwa anageuka, uso kwa uso na mtu akiwa amevaa kama mtu bara la Asia akiwa amekaa chini. Daktari Mbaga alimwangalia huyo mtu kama akimfananisha kuna sehemu aliwai kumuona lakini mboni za macho yake yalimthibitishia akuwai kumuona sehemu yeyote hapo ndio mara yake ya kwanza kumuona. 

          Mtu huyo alisimama anasogea hadi alipo Daktari Mbaga kwa mwendo wa taratibu kutokana na umri umeenda mwenye mvi kichwani zinazoonekana kwa mbali chini ya mwisho wa kofia aliovaa. Huyo mtu alifika hadi alipo daktari Mbaga, daktari Mbaga alitoa begi mkono wa kulia anashika mkono wa kushoto kwa ajiri ya kusalimiana lakini huyo tu alinyoosha mkono wa  kushoto.

“Asalam Aleykhum”

          Daktari Mbaga ni mkatoliki tangu kuzaliwa kwake lakini dini ya kiislamu anaifahamu kupitia eneo analokaa hata salamu zao waislamu anazifahamu kwa kuwaona wakisalimiana lakini alishangaa salamu inayotoka kwa huyo mtu ni ya kiislamu lakini alinyoosha mkono wa kushoto, wakati anajua ni mkono wa kulia, sio waislamu tu salamu yeyote lazima utoe mkono wa kulia.

          Akutaka kumuuliza  lakini imani yake daktari Mbaga ilisadiki huyo mtu amechanganyikiwa uenda anauguliwa na mgonjwa wake imepelekea kuvurugwa hadi anatoa salamu kwa mkono wa kushoto. Akutaka kumjaji sana huyo mtu, aliitikia salamu kama waislamu wanavyoitikia na anamuamkia kama mkubwa kwake na alitulia kumsikiliza. Mtu huyo alikohoa kidogo kulainisha koo na anamwangalia kwa muda daktari Mbaga na anamshika bega alimwambia kwa sauti ya chini na ilioshiria utu uzima.

“Bila shaka wewe ndio daktari bingwa wa uchunguzi wa maiti na muda huu unawai katika chumba cha vipimo,sasa najua umesomea unachokwenda kukipima kwa hiyo kuna maiti mbili zitafika muda huu, naomba hizo maiti utoe vipimo sahihi na usithubutu kutoa vipimo vya uongo vitaghalimu maisha yako.”


         *************ITAENDELEA IJUMAA IJAYO ************

MAWASILIANO ZAIDI TUCHEKI KUPITIA NAMBA HII KWA KUTUTUMIA HABARI +255682842818

Chapisha Maoni

0 Maoni